Friday, April 1, 2016

EWURA yashusha bei ya umeme na kufuta Service Charge


Leo kitendawili kimeteguliwa baada ya Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji EWURA kutangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.

Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kutaka bei za umeme zipunguzwe. Sambamba na ushushwaji wa bei za umeme gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa. 
Bei mpya  kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292  toka  298  ya  zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200  ya  hapo  awali.

Bei mpya  kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152  toka  sh. 156  ya  hapo awali.
Hii ni habari njema sana kwa watumiaji wa nisahti ya umeme.

No comments: