Thursday, March 31, 2016

Nchi zingine 10 zasitisha Misaada TANZANIA

Nchi 10 kati ya 14 za Umoja wa Ulaya Zatangaza kusitisha Ufadhili wao Kwa Bajeti ya Serikali ya Tanzania Kisa ni marudio ya uchaguzi wa Zanzibar uliofanyika hivi majuzi.

Tamko hilo limetoka ikiwa ni mwendelezo wa tamko lililo tokea March 29 2016 na bodi ya shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC) ilisitisha msaada wa awamu ya pili wa kutotoa zaidi dola 472 sawa na Trilioni 1.4 za kitanzania kwa Tanzania kutokana na kile lilichosema kuwa ni kufanyika kwa uchaguzi Zanzibar licha ya malalamiko ya uchaguzi huo lakini pia sheria mpya ya makosa ya mitandao Tanzania.
Shirika la utangazaji la Uingereza BBC kupitia bbcswahili.com limeandika ripoti ifuatayo 'kundi la watoa misaada 10 kutoka nchi za magharibi limetangaza kusitisha ufadhili wao kwa bajeti ya serikali ya Tanzania, hii inafuatia uamuzi wa shirika la utoaji misaada la serikali ya Marekani kuondoa msaada kutokana na uchaguzi wa Zanzibar ulivyoendeshwa'
Ikumbukwe kuwa zaidi ya asilimia 10  ya bajeti ya Tanzania inategemea msaada mwaka huu wa fedha, kwa hivyo hatua hizo za hivi punde ni pigo kwa mipango ya maendeleo ya serikali mpya ya Mhe. Dr. J. P. Magufuli

BREAKING NEWS: Wabunge watatu wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za Rushwa

Ni tetesi zilizokuwa zinashika kasi kwenye mitandao ya kijamii zikisema wabunge kadhaa wa kamati ya kudumu ya bunge ya HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA.
Wabunge hao wamefikishwa Mahakamani Kisutu Dar es salaam mchana wa March 31 2016 kwa tuhuma za rushwa, Victor Mwambalaswa wa Lupa (CCM), Kangi Lugola wa Mwibara (CCM) na Sadiq Murad wa Mvomero (CCM) na ripoti zinasema waliomba rushwa ya TZS 30 MILIONI.

Video hii hapa kutoka millardayo.com jionee mwenyewe.

Kutokana na taarifa hii pia chama cha mapinduzi kime sikitishwa na tuhuma hizi kwa wabunge wake ambapo Msemaji wa chama hicho Ndugu Christopher Ole-Sendeka   ametoa ufafanuzi kuhusu suala la rushwa na hatua zinazoendelea huku akisikitishwa na tabia ya wabunge kujihusishwa na tabia hiyo

Barua hiyo imeabatanishwa hapa chini.

Kilimo cha MAPAPAI Kinalipa !!!

HEBU CHUKUA KALUKUKETA YAKO, TUFANYE HESABU..!!

Eka moja ya shamba la papai inaweza kuingiza miche 1000-1200(elfu moja hadi elfu na mia mbili)-zile mbegu fupi. 
  • Tufanye umepanda miche 1,000. Mti mmoja ukiuhudumia vema unaweza kutoa matunda hadi 120 kwa msimu. 
  • Tufanye umetoa matunda 80, tu. Tunda moja kwa bei ya shamba tufanye umeuza bei ya "kutupwa" ya Tsh. 500/= (lakini papai lililoshiba linauzwa hadi Tsh. 3,000/= sokoni). Chukua 500/= mara 80 unapata 40,000/=(elfu arobaini kwa mti mmoja). 
  • Sasa chukua 40,000/= zidisha mara 1,000 unapata 40,000,000/=(milioni arobaini). 
  • Gharama za kulima papai ekari moja haizidi milioni mbili. 


Sunday, March 6, 2016

Mh. Rais atangaza uteuzi wa katibu mkuu kiongozi mpya




Leo tarehe 6.3.2016 Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amemtangaza katibu mkuu kiongozi mpya kwenye serikali yake Mhandisi John Kijazi ambaye anachukua nafasi hiyo iliyokua kwa Ombeni Sefue, katibu mkuu mpya Mhandisi John Kijazi amekua akifanya kazi kama Balozi wa Tanzania India, mtazame Rais Magufuli hapa chini.



Rais J. P. Magufuli akimshukuru Balozi Ombeni Sefue kwa mchango wake na uchapoa kazi katika miezi yake mitatu ya uongozi.
Katika uteuzi huu Mh. Rais amesema Balozi Sefue atampangia kazi nyingine.