Thursday, March 31, 2016

BREAKING NEWS: Wabunge watatu wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za Rushwa

Ni tetesi zilizokuwa zinashika kasi kwenye mitandao ya kijamii zikisema wabunge kadhaa wa kamati ya kudumu ya bunge ya HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA.
Wabunge hao wamefikishwa Mahakamani Kisutu Dar es salaam mchana wa March 31 2016 kwa tuhuma za rushwa, Victor Mwambalaswa wa Lupa (CCM), Kangi Lugola wa Mwibara (CCM) na Sadiq Murad wa Mvomero (CCM) na ripoti zinasema waliomba rushwa ya TZS 30 MILIONI.

Video hii hapa kutoka millardayo.com jionee mwenyewe.

Kutokana na taarifa hii pia chama cha mapinduzi kime sikitishwa na tuhuma hizi kwa wabunge wake ambapo Msemaji wa chama hicho Ndugu Christopher Ole-Sendeka   ametoa ufafanuzi kuhusu suala la rushwa na hatua zinazoendelea huku akisikitishwa na tabia ya wabunge kujihusishwa na tabia hiyo

Barua hiyo imeabatanishwa hapa chini.




No comments: